Jumamosi, Agosti 20, 2016

SIMBA YAANZA KUGAWA DOZI VPL


Simba Sc leo imeanza ligi vyema kwa kuitandika timu ya Ndanda goli 3 - 1 katika mchezo uliochezwa leo katika uwanja wa Taifa.


Magoli ya Simba yamefungwa na wachezaji wageni Laudit Mavugo, Fredrick Blagnon na Shiza Kichuya.

Katika michezo mingine Timu za Stand United na Mbao FC zimetoka sare ya kutofungana katika Uwanja wa CCM Kambarage - Shinyanga, wakata miwa wa Mtibwa wamepokea kichapo cha goli 1 kutoka kwa Ruvu Shooting ya Masau Bwire. Nao Prison wameshinda goli moja dhidi ya Majimaji kule Songea.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni